Baadhi ya wanachama wa IPC wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waliochaguliwa kuongoza IPC ,mwenye pama katikati ni mmiliki wa mtandao huu Bw Francis Godwin ambaye alipita bila kupingwa katika nafasi ya ukatibu msaidizi wa IPC
Katika uchaguzi huu viongozi walioanguka katika uchaguzi huo ambao walikuwemo katika safu ya uongozi katika uongozi uliopita ni pamoja na Sima Bingileki ambaye alikuwa makamu mwenyekiti,huku Eliasa Ally ambaye alikuwa mjumbe kipindi kilichopita akijitoa kugombea tena nafasi hiyo na Kenneth Simbaya akiamua kustaafu nafasi ya kiti pamoja na Hakimu Mwafongo ambaye hakugombea tena nafasi ya ukatibu msaidizi .
Katiba nafasi ya uweka hazina msaidizi Vicky Macha wa Nipashe Iringa alipita bila kupingwa huku nafasi ya katibu msaidizi pia Francis Godwin mwandishi wa gazeti la Tanzania daima Irina ,kurugenzi wa kampuni ya Free Community Media's na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari za jinsia Tanzania (TGNP) mikoa ya kusini akipita bila kupingwa pamoja na wajumbe 13 7 wa kamati ya utendaji ndani ya IPC pia wakipita bila kupingwa kufuatia Eliasa Ally kujitoa katika kinyang'anyiro hicho.
Wajumbe 13 wanaounda kamati ya utendaji ndani ya IPC ni pamoja na Daud Mwangosi, Frank Leonard ,Zulfa Shomary, Francis Godwin, Suleman Boki,Vicky Macha, Getrude Madembwe, Shabani Lupimo, Frederick Siwale,Conard Mpila,Fulgence Malangalila,Janeth Matondo na Jackson Manga .
UMOJA NDIO NGUZO YETU. Bomba FM 104.0MHz, Generation FM 89.9MHz,Baraka FM 107.6MHz, Ushindi FM 98.6MHz, Rock FM 93.2MHz, Mbeya FM 89.5MHz, Sweet FM,na Mbeya Highlands FM 92.7
Sunday, July 31, 2011
KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM CHAFUNGULIWA LEO MJINI DODOMA, AMBAPO MENGI YANATARAJIWA KUJITOKEZA KTK KIKAO HICHO
Mwenyekiti wa CCM taifa, Jakaya Kikwete, Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar, Aman Abeid Karume (wa tatu kushoto), Rais wa Zanzibar, Dkt Ali Mohamed Shein na Mwenyekiti wa CCM Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi (kushoto), Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa (kulia) na Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Willson Mukama, wakiwa katika ufunguzi wa Kikao cha Kamati kuu kilichofunguliwa leo Julai 31, katika Ukumbi wa CCM Makao Makuu mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, akiingia katika Ukumbi wa CCM Makao Makuu mjini Dodoma, leo Julai 31, wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Kamati kuu. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Willson MukamaMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika ufunguzi wa Kikao cha Kamati Kuu kilichoanza leo Julai 31, 2011 katika Ukumbi wa CCM Makao Makuu mjini Dodoma. Katikati ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
WAANDISHI WA HABARI MACHACHARI MKOANI MBEYA KWA MWAKA 2007
Hawa ni waandishi wa habari mkoani mbeya kwa miaka minne iliyopita wakiwa nje ya Ukumbi wa Mkutano wa MKAPA uliopo jijini Mbeya na kupiga picha ya pamoja.
Ukiwa tazama siku hizi ni tofauti na maumbile yao walivyokuwa hapo awali, Je? Nini maoni yako?
Saturday, July 30, 2011
WAZAZI WAPINGA KITENDO CHA KUTOA MCHANGO WA CHAKULA MBATA JIJINI MBEYA
Wazazi wa mtaa wa Mbata kata ya Ghana jijini Mbeya wamepinga kitendo cha kutoa mchango wa chakula kwa wanafunzi sio kigezo cha kuboresha kiwango cha kufaulu kwa wanafunzi katika shule za msingi.
Wakijadili katika mkutano wa wazazi uliofanyika shule ya msingi Mbata wazazi hao wamesema wizara ya elimu inatakiwa kuangalia njia nyingine inayoweza kuwafanya wanafunzi kumudu masomo yao na si kwa kutumia kigezo cha chakula mashuleni.
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Mbata Agabo Mwakatobe amewataka wazazi kuchangia gharama za chakula kwa watoto wao kwa kuwa wanafunzi wanapokuwa na njaa hawatoweza kusikiliza wanachofundishwa na waalimu wao.
Hivi karibuni wananchi waliilalamikia Serikali kushindwa kutoa chakula mashuleni, lakini baada ya Serikali kukubali mpango wa chakula mashuleni wazazi wameanza kupingana kuhusu mpango huo.
HALI YA MIUNDOMBINU BADO NI TETE MBEYA VIJIJINI
Wakazi wa vitongoji vya DDC, Mtakuja na Mlima Reli wilaya ya Mbeya Vijijini wanalazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 7 kutafuta huduma ya maji safi na salama.
Wakazi hao wamesema kutokana na tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama wamekuwa wakilazimika kutumia maji ya Mto Mbalizi ambayo maji yake ni machafu na sio salama kwa matumizi ya binadamu.
Mmoja wa wanakijiji hao Michael Mwaifwani amesema licha ya kuwepo kwa miundombinu ya maji katika vitongoji hivyo bado upatikanaji wa huduma hiyo imekuwa ni tabu na kwamba wamekuwa wakilazimika kulipa bili ya maji ya shilingi elfu kumi kila mwezi.
Naye mwenyekiti wa kitongoji cha DCC bwana Joined Mwalusanya amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa ongezeko la wakazi ni moja ya sababu inayopelekea utoaji wa huduma hiyo kusua sua.
BEI ZA MAZAO ZA BADIRIKA MARA KWA MARA SOKO LA SIDO MWANJELWA MBEYA.
Bei za mazao ya vyakula katika soko la Sido Mwanjelwa jijini mbeya zimekuwa zikibadilika mara kwa mara kutokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji na usafirishaji.
Mmoja wa wafanyabishara sokoni hapo bwana James Fredrick amesema debe la nyanya imepanda kutoka shilingi elfu 10 hadi kufikia shilingi elfu 12 kwa sasa.
Naye Lugano Mwakalundwa amesema bei ya mahindi imepanda kutoka shilingi elfu 33 kwa gunia hadi kufikia shilingi elfu 36 na kwamba kuna uwezekano wa bei hiyo kuendelea kupanda kutokana na mahitaji makubwa ya chakula hicho kwa mikoa mingine ambayo inakabiliwa na tatizo la njaa.
Kwa hisani ya CHIMBUKO LETU Bloguhttp://ukurasampyahuu.blogspot.com/
Wakijadili katika mkutano wa wazazi uliofanyika shule ya msingi Mbata wazazi hao wamesema wizara ya elimu inatakiwa kuangalia njia nyingine inayoweza kuwafanya wanafunzi kumudu masomo yao na si kwa kutumia kigezo cha chakula mashuleni.
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Mbata Agabo Mwakatobe amewataka wazazi kuchangia gharama za chakula kwa watoto wao kwa kuwa wanafunzi wanapokuwa na njaa hawatoweza kusikiliza wanachofundishwa na waalimu wao.
Hivi karibuni wananchi waliilalamikia Serikali kushindwa kutoa chakula mashuleni, lakini baada ya Serikali kukubali mpango wa chakula mashuleni wazazi wameanza kupingana kuhusu mpango huo.
HALI YA MIUNDOMBINU BADO NI TETE MBEYA VIJIJINI
Wakazi wa vitongoji vya DDC, Mtakuja na Mlima Reli wilaya ya Mbeya Vijijini wanalazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilometa 7 kutafuta huduma ya maji safi na salama.
Wakazi hao wamesema kutokana na tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama wamekuwa wakilazimika kutumia maji ya Mto Mbalizi ambayo maji yake ni machafu na sio salama kwa matumizi ya binadamu.
Mmoja wa wanakijiji hao Michael Mwaifwani amesema licha ya kuwepo kwa miundombinu ya maji katika vitongoji hivyo bado upatikanaji wa huduma hiyo imekuwa ni tabu na kwamba wamekuwa wakilazimika kulipa bili ya maji ya shilingi elfu kumi kila mwezi.
Naye mwenyekiti wa kitongoji cha DCC bwana Joined Mwalusanya amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa ongezeko la wakazi ni moja ya sababu inayopelekea utoaji wa huduma hiyo kusua sua.
BEI ZA MAZAO ZA BADIRIKA MARA KWA MARA SOKO LA SIDO MWANJELWA MBEYA.
Bei za mazao ya vyakula katika soko la Sido Mwanjelwa jijini mbeya zimekuwa zikibadilika mara kwa mara kutokana na kupanda kwa gharama za uzalishaji na usafirishaji.
Mmoja wa wafanyabishara sokoni hapo bwana James Fredrick amesema debe la nyanya imepanda kutoka shilingi elfu 10 hadi kufikia shilingi elfu 12 kwa sasa.
Naye Lugano Mwakalundwa amesema bei ya mahindi imepanda kutoka shilingi elfu 33 kwa gunia hadi kufikia shilingi elfu 36 na kwamba kuna uwezekano wa bei hiyo kuendelea kupanda kutokana na mahitaji makubwa ya chakula hicho kwa mikoa mingine ambayo inakabiliwa na tatizo la njaa.
Kwa hisani ya CHIMBUKO LETU Bloguhttp://ukurasampyahuu.blogspot.com/
Friday, July 29, 2011
JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA KUENDELEA KUFANYA UCHUNGUZI WA MGOGORO
JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA KUENDELEA KUFANYA UCHUNGUZI WA MGOGORO
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mbeya ADVOCATE NYOMBI amesema jeshi lake linaendea na uchunguzi ili kubaini ukweli wa mgogoro kati ya wananchi wa kijiji cha kapunga wilayani Mbarali mkoani Mbeya dhidi ya mwekezaji wa kampuni Rice Project
Kuhusu vitendo vya uharibifu wa mali za wananchi Kamanda NYOMBI amesema hana taarifa nazo na kwamba na kuwataka wananchi hao kuwa watulivu wakati uchunguzi ukiendelea.
Hata hivyo habari tulizozipata zinadai kuwa mwekezaji huyo alivunja matofali kumi na mbili elfu ambayo yalifyatuliwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Mbarali na kumjeruhi mwanakijiji kwa kumgonga na gari.
MAITI YA MTOTO MCHANGA YATUPWA JALALANI MBEYA.
Maiti ya mtoto mchanga imekutwa ndani ya mfuko wa Rambo uliotupwa kwenye dampo la shule ya msingi ya Sinde liliyopo kata ya Ruanda mtaa mtoni jijini Mbeya.
Habari za kukutwa kwa maiti ya mtoto mchanga zimetolewa na watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi ambao walikuwa wanaokota mifuko hiyo kwenye dampo hilo kwa ajili ya kwenda kuziuza kwa wafanyabiashara wa mkaa.
Imeeleza kuwa baada ya watoto hao kuifungua Rambo ndipo walipokutana na maiti ya mtoto mchanga na kutoa taarifa kwa wafanyabiashara na wakazi wa mtaa wa Mtoni ambao nao walitoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Hata hivyo hakuna mtu anayehisiwa kwenye mtaa huo kuhusika na tukio la kutupwa kwa maiti hiyo, Jeshi la polisi lilifika eneo hilo majira ya saa mbili za usiku na kuondoka na mwili wa mtoto huyo ambaye anadaiwa kuwa na siku moja tangu azaliwe.
UKOSEFU WA VITENDEA KAZI KITUO CHA AFYA NSONYANGA - MBARALI
Kituo cha afya cha Nsonyanga kilichopo kijiji cha Kapyo kata ya mahongole wilayani mbarali mkoani Mbeya kinakabiliwa na upungufu mkubwa wa vitendea kazi, usafiri kwa ajili ya wagonjwa, nyumba za watumishi na upatikanaji wa nishati ya umeme.
Mkuu wa kituo hicho Dakta EDSON MWANDEUKA amesema wanalazimika kutumia taa ya Chemli wakati wa kutoa huduma za uzazi kwa wakina mama wajawazito nyakati za usiku hali inayohatarisha usalama wa afya kwa wakina mama hao.
Kutokana na tatizo hilo mwenyekiti wa kijiji hicho bwana KYANDO amesema uongozi wa kijiji chake unaendelea na mchakato wa kufanikisha kituo hicho kinapata nishati ya Umeme ili kurahisisha zoezi la utoaji wa huduma kwa wagonjwa nyakati za usiku.
Kituo cha Nsonyanga kina wauguzi 3 ambapo kituo hicho kinahudumia vijiji vya kapyo, uswisi, ilongo, Nsonyanga, azimio mapula, malawato na mkoi.
MAONYESHO YA KILIMO MWAKA HUU MKOANI MBEYA YAVUNJA REKODI.
Maonesho ya Kilimo ya mwaka huu yamevunja rekodi ya mwaka jana baada ya kujitokeza wadau wapatao 400 watakaoshiriki kwenye maonesho hayo ikilinganishwa na ya mwaka jana ambayo wadau takriban 300 ndio walioshiriki maonesho hayo.
Kwa upande wa miundo mbinu KASILATI amesema TASO imejiandaa kuhakikisha barabara zinachongwa vizuri, huduma za Afya zinatolewa uwanjani humo, maji yanapatikana licha ya changamoto ya nishati ya Umeme kuwepo.
Aidha Bwana KASILATI ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika maonesho hayo yatakayoanza rasmi tarehe moja mwezi wa Nane.
UZOAJI TAKATAKA WAENDELEWA KUSUASUA MJI MDOGO WA MBALIZI MBEYA VIJIJINI.
Wafanyabiashara wa soko la Tarafani Mbalizi Wilaya ya Mbeya vijijini wameulalamikia uongozi wa soko hilo kwa kushindwa kutoa takataka zilizojaa kwenye Dampo la soko hilo kwa mda mrefu.
Wamesema halmashauri ya wilaya hiyo haina utaratibu wa kuzoa na kutupata taka pindi zinapo jaa kwenye dampo hali inayopelekea kuwepo kwa harufu mbaya sokoni hapo.
Mmoja wa wafanyabishara wa soko hilo RASHIND EFRAIMU amesema wamekuwa wakilipia ushuru kila siku na kwamba kinachowakera ni kuona takataka zikiendelea kurundikana kwenye dampo ikiwa ni pamoja na miundombinu ya soko kuendelea kuwa mibovu.
Nao wauzaji wa chakula wameuomba uongozi wa halmashauri ya Mbeya Vijijini kuchukuwa hatua za haraka za kuondoa taka kwenye madampo ili kuondoa kero ya harufu mbaya inayopelekea kukimbiwa na wateja.
Afisa afya wa soko hilo MHEMEJI amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa uchache wa magari ya kubebea taka ndio sababu ya kusuasua kwa zoezi la uzoaji wa taka.
Kwa hisani ya CHIMBUKO LETU Blogu http://ukurasampyahuu.blogspot.com/
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mbeya ADVOCATE NYOMBI amesema jeshi lake linaendea na uchunguzi ili kubaini ukweli wa mgogoro kati ya wananchi wa kijiji cha kapunga wilayani Mbarali mkoani Mbeya dhidi ya mwekezaji wa kampuni Rice Project
Kuhusu vitendo vya uharibifu wa mali za wananchi Kamanda NYOMBI amesema hana taarifa nazo na kwamba na kuwataka wananchi hao kuwa watulivu wakati uchunguzi ukiendelea.
Hata hivyo habari tulizozipata zinadai kuwa mwekezaji huyo alivunja matofali kumi na mbili elfu ambayo yalifyatuliwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Mbarali na kumjeruhi mwanakijiji kwa kumgonga na gari.
MAITI YA MTOTO MCHANGA YATUPWA JALALANI MBEYA.
Maiti ya mtoto mchanga imekutwa ndani ya mfuko wa Rambo uliotupwa kwenye dampo la shule ya msingi ya Sinde liliyopo kata ya Ruanda mtaa mtoni jijini Mbeya.
Habari za kukutwa kwa maiti ya mtoto mchanga zimetolewa na watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi ambao walikuwa wanaokota mifuko hiyo kwenye dampo hilo kwa ajili ya kwenda kuziuza kwa wafanyabiashara wa mkaa.
Imeeleza kuwa baada ya watoto hao kuifungua Rambo ndipo walipokutana na maiti ya mtoto mchanga na kutoa taarifa kwa wafanyabiashara na wakazi wa mtaa wa Mtoni ambao nao walitoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Hata hivyo hakuna mtu anayehisiwa kwenye mtaa huo kuhusika na tukio la kutupwa kwa maiti hiyo, Jeshi la polisi lilifika eneo hilo majira ya saa mbili za usiku na kuondoka na mwili wa mtoto huyo ambaye anadaiwa kuwa na siku moja tangu azaliwe.
UKOSEFU WA VITENDEA KAZI KITUO CHA AFYA NSONYANGA - MBARALI
Kituo cha afya cha Nsonyanga kilichopo kijiji cha Kapyo kata ya mahongole wilayani mbarali mkoani Mbeya kinakabiliwa na upungufu mkubwa wa vitendea kazi, usafiri kwa ajili ya wagonjwa, nyumba za watumishi na upatikanaji wa nishati ya umeme.
Mkuu wa kituo hicho Dakta EDSON MWANDEUKA amesema wanalazimika kutumia taa ya Chemli wakati wa kutoa huduma za uzazi kwa wakina mama wajawazito nyakati za usiku hali inayohatarisha usalama wa afya kwa wakina mama hao.
Kutokana na tatizo hilo mwenyekiti wa kijiji hicho bwana KYANDO amesema uongozi wa kijiji chake unaendelea na mchakato wa kufanikisha kituo hicho kinapata nishati ya Umeme ili kurahisisha zoezi la utoaji wa huduma kwa wagonjwa nyakati za usiku.
Kituo cha Nsonyanga kina wauguzi 3 ambapo kituo hicho kinahudumia vijiji vya kapyo, uswisi, ilongo, Nsonyanga, azimio mapula, malawato na mkoi.
MAONYESHO YA KILIMO MWAKA HUU MKOANI MBEYA YAVUNJA REKODI.
Maonesho ya Kilimo ya mwaka huu yamevunja rekodi ya mwaka jana baada ya kujitokeza wadau wapatao 400 watakaoshiriki kwenye maonesho hayo ikilinganishwa na ya mwaka jana ambayo wadau takriban 300 ndio walioshiriki maonesho hayo.
Kwa upande wa miundo mbinu KASILATI amesema TASO imejiandaa kuhakikisha barabara zinachongwa vizuri, huduma za Afya zinatolewa uwanjani humo, maji yanapatikana licha ya changamoto ya nishati ya Umeme kuwepo.
Aidha Bwana KASILATI ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika maonesho hayo yatakayoanza rasmi tarehe moja mwezi wa Nane.
UZOAJI TAKATAKA WAENDELEWA KUSUASUA MJI MDOGO WA MBALIZI MBEYA VIJIJINI.
Wafanyabiashara wa soko la Tarafani Mbalizi Wilaya ya Mbeya vijijini wameulalamikia uongozi wa soko hilo kwa kushindwa kutoa takataka zilizojaa kwenye Dampo la soko hilo kwa mda mrefu.
Wamesema halmashauri ya wilaya hiyo haina utaratibu wa kuzoa na kutupata taka pindi zinapo jaa kwenye dampo hali inayopelekea kuwepo kwa harufu mbaya sokoni hapo.
Mmoja wa wafanyabishara wa soko hilo RASHIND EFRAIMU amesema wamekuwa wakilipia ushuru kila siku na kwamba kinachowakera ni kuona takataka zikiendelea kurundikana kwenye dampo ikiwa ni pamoja na miundombinu ya soko kuendelea kuwa mibovu.
Nao wauzaji wa chakula wameuomba uongozi wa halmashauri ya Mbeya Vijijini kuchukuwa hatua za haraka za kuondoa taka kwenye madampo ili kuondoa kero ya harufu mbaya inayopelekea kukimbiwa na wateja.
Afisa afya wa soko hilo MHEMEJI amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa uchache wa magari ya kubebea taka ndio sababu ya kusuasua kwa zoezi la uzoaji wa taka.
Kwa hisani ya CHIMBUKO LETU Blogu http://ukurasampyahuu.blogspot.com/
Thursday, July 28, 2011
VITUKO BUNGENI JAMANI SI VYA KUVIFUMBIA MACHO KAMA WANANCHI
Mbunge wa Nyamagana (CHADEMA) Ezekia Wenje (aliyevaa suti ya rangi ya maziwa) akitolewa nje ya ukumbi wa Bunge na Askari Polisi wa Bunge baada ya kutomtii Mwenyekiti wa kikao cha Bunge cha leo Mbunge wa Dole (CCM) Silvester Mabumba, alimtaka kukaa chini na kutokutoa hoja ya dharula kuhusu Samaki wa sumu kutoka
Mbunge wa Nyamagana (CHADEMA) Ezekia Wenje (aliyevaa suti ya rangi ya maziwa) akitolewa nje ya ukumbi wa Bunge na Askari Polisi wa Bunge.
Mbunge wa Ludewa (CCM) Deo Filikunjombe (kushoto) akisutwa nje ya ukumbi wa Bunge na baadhi ya wabunge wa upinzani Moses Machari (kulia), Philipa Mturano (katikati) na Ezekia Wenje (kushoto) baada ya Filikunjombe kumwambia Wenje kuwa alikosa ustaarabu kwa kutokumtii Mwenyekiti wa kikao cha Bunge cha leo Mbunge wa Dole (CCM) Silvester Mabumba pale alipomwambia akae chini na kutokutoa hoja ya dharula kuhusu samaki wa sumu kutoka Japan.
Baadhi ya mawaziri wakimpongea waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Prof. Jummanne Maghembe mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya wizara yake jana jioni katika kikao cha Bunge la bajeti kinachoendelea mjini Dodoma.
NJE YA UKUMBI WA BUNGE
bunge wa Ludewa (CCM) Deo Filikunjombe (kushoto) akisutwa nje ya ukumbi wa Bunge na Mbunge wa viti Maalum (CHADEMA) Suzan Kiwanga (aliyevaa kitenge) baada ya Filikunjombe kumwambia, Ezekia Wenje, mbunge wa Nyamagana (CHADEMA) (hayupo pichani) alikosa ustaarabu kwa kutokumtii Mwenyekiti wa kikao cha Bunge cha leo Mbunge wa Dole (CCM) Silvester Mabumba pale alipomwambia akae chini na kutokutoa hoja ya dharula kuhusu Samaki wa sumu kutoka Japan.
Mbunge wa Ludewa (CCM) Deo Filikunjombe (kulia) akisutwa nje ya ukumbi wa Bunge na wabunge wa viti Maalum (CHADEMA) Philipa Mturano (kushoto) Suzan Kiwanga (aliyevaa kitenge) na Mbunge wa jimbo la Kasulu mjini (NCCR – MAGEUZI) Moses Machari.
Mbunge wa Nyamagana (CHADEMA) Ezekia Wenje (aliyevaa suti ya rangi ya maziwa) akitolewa nje ya ukumbi wa Bunge na Askari Polisi wa Bunge.
Mbunge wa Ludewa (CCM) Deo Filikunjombe (kushoto) akisutwa nje ya ukumbi wa Bunge na baadhi ya wabunge wa upinzani Moses Machari (kulia), Philipa Mturano (katikati) na Ezekia Wenje (kushoto) baada ya Filikunjombe kumwambia Wenje kuwa alikosa ustaarabu kwa kutokumtii Mwenyekiti wa kikao cha Bunge cha leo Mbunge wa Dole (CCM) Silvester Mabumba pale alipomwambia akae chini na kutokutoa hoja ya dharula kuhusu samaki wa sumu kutoka Japan.
Baadhi ya mawaziri wakimpongea waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Prof. Jummanne Maghembe mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya wizara yake jana jioni katika kikao cha Bunge la bajeti kinachoendelea mjini Dodoma.
NJE YA UKUMBI WA BUNGE
bunge wa Ludewa (CCM) Deo Filikunjombe (kushoto) akisutwa nje ya ukumbi wa Bunge na Mbunge wa viti Maalum (CHADEMA) Suzan Kiwanga (aliyevaa kitenge) baada ya Filikunjombe kumwambia, Ezekia Wenje, mbunge wa Nyamagana (CHADEMA) (hayupo pichani) alikosa ustaarabu kwa kutokumtii Mwenyekiti wa kikao cha Bunge cha leo Mbunge wa Dole (CCM) Silvester Mabumba pale alipomwambia akae chini na kutokutoa hoja ya dharula kuhusu Samaki wa sumu kutoka Japan.
Mbunge wa Ludewa (CCM) Deo Filikunjombe (kulia) akisutwa nje ya ukumbi wa Bunge na wabunge wa viti Maalum (CHADEMA) Philipa Mturano (kushoto) Suzan Kiwanga (aliyevaa kitenge) na Mbunge wa jimbo la Kasulu mjini (NCCR – MAGEUZI) Moses Machari.
WANAFUNZI WAGEUZWA NAWAALIMU KUWA WAFANYAKAZI WA NDANI MAENEO YA VIJIJINI
Wanafunzi wa shule ya Msingi Manda wilaya ya Ludewa wakitoka kuokota kuni za kuuza ili kupata fedha za mchango wa mitihani
Wanafunzi wa kike katika shule ya msingi Manda wilaya ya Ludewa ambao wanasubiri kufanya mtihani wa Taifa wa Darasa la saba wakitoka kuokota kuni porini mida ya masomo baada ya kufukuzwa kwa kushindwa kulipa mchango wa shilingi 600 ili wapate kufanya mitihani ya kujipima ya kata mzigo wa kuni kama huu wamekuwa wakiuuza kwa kiasi cha shilingi 100 kwa walimu wao
Afisa elimu wa wilaya ya Ludewa Bw.Yella akiwahoji wanafunzi shule ya msingi Manda ambao walikutwa wakitoka kuvua samaki wakati wa masomo baada ya kufukuzwa na walimu kwa kushindwa kulipa mchango wa shilingi 600 wa mtihani wa kata
Wakati haya yakijitokeza huko Ludewa jamii inatakiwa kijitathimini mara mbili kuangalia namna ambavyo tunaweza kudhibiti vitendo hivyo ili kuwawezesha wanafunzi kutumia muda wao vizuri ktk masomo yao
Wanafunzi wa kike katika shule ya msingi Manda wilaya ya Ludewa ambao wanasubiri kufanya mtihani wa Taifa wa Darasa la saba wakitoka kuokota kuni porini mida ya masomo baada ya kufukuzwa kwa kushindwa kulipa mchango wa shilingi 600 ili wapate kufanya mitihani ya kujipima ya kata mzigo wa kuni kama huu wamekuwa wakiuuza kwa kiasi cha shilingi 100 kwa walimu wao
Afisa elimu wa wilaya ya Ludewa Bw.Yella akiwahoji wanafunzi shule ya msingi Manda ambao walikutwa wakitoka kuvua samaki wakati wa masomo baada ya kufukuzwa na walimu kwa kushindwa kulipa mchango wa shilingi 600 wa mtihani wa kata
Wakati haya yakijitokeza huko Ludewa jamii inatakiwa kijitathimini mara mbili kuangalia namna ambavyo tunaweza kudhibiti vitendo hivyo ili kuwawezesha wanafunzi kutumia muda wao vizuri ktk masomo yao
Subscribe to:
Posts (Atom)








