Katibu Mkuu, Phillemon Luhanjo, akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma ambapo alitangaza rasmi kusimamishwa kazi kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, kufuatia kashfa zinazomuandama hivi sasa.
Picha ya Kukopi katika moja ya gazeti, Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, amesimamishwa kazi rsmi kufuatia kutangazwa rasmi habari hizo na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemo Luhanjo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma Julai 21 mchana.
UMOJA NDIO NGUZO YETU. Bomba FM 104.0MHz, Generation FM 89.9MHz,Baraka FM 107.6MHz, Ushindi FM 98.6MHz, Rock FM 93.2MHz, Mbeya FM 89.5MHz, Sweet FM,na Mbeya Highlands FM 92.7
Friday, July 22, 2011
MAGARI MAWILI YATEKETEA KWA MOTO MARA BAADA YA KUGONA USO KWA USO
HIVI NDIVYO GARI LA HOOD LINAVYOONEKANA BAADA YA KUTEKETEA KWA MOTO
HAPA NI GARI LA HOOD NA GARI LA MIZIGO LIKIWAKA MOTO MARA BAADA YA KUGONGANA KATIKA ENEO LA MIKUMI MKOANI MOROGORO
HAPA NI GARI LA HOOD NA GARI LA MIZIGO LIKIWAKA MOTO MARA BAADA YA KUGONGANA KATIKA ENEO LA MIKUMI MKOANI MOROGORO
BASI LA HOOD LATEKETEA KWA MOTO LAUA 5 NA KUJERUHI 41
hivi ndivyo hali ilivyotokea baada ya basi la Hood lililokuwa likitoka Mkoani Mbeya kwenda Arusha,lilipogongana uso kwa uso na lori la mizigo lilolokuwa na mafuta ya kula tani 24 kutoka Morogoro kwenda Songea kwenye barabara iliyopo ndani ya hifandi ya Taifa ya Mikuki,mkoani Morogoro.watu watano walifariki na 41 kujeruhiwa.
UKWELI WAPATIKANA KWA DIWANI WA CHADEMA KUHAMIA CCM - NZOVWE MBEYA
Zikiwa zimepita siku 3 tangu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kusema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimedanganya Umma katika mkutano wake kwa kusema Diwani wa kata ya Nzovwe EZIRONI MWAKALOBO kupitia Chadema amejihuzulu na kuhamia CCM hatimae viongozi hao wamebadilisha usemi kwa kukubali kuwa kilichoongelewa ni kweli.
Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Mbeya mjini JOHN MWAMBIGIJA amesema pamoja na jitihada za uongozi wa chama chake kushinikiza kukanusha barua ya kujihuzulu wadhifa wake bado EZIRONI MWAKALOBO ameendelea na msimamo wake wa kung’atuka madarakani.
Aidha MWAMBIGIJA amesema mpango wa CHADEMA hivi sasa ni kujipanga katika kuhakikisha wanachukua tena kiti cha Udiwani kata hiyo mara baada ya kutangazwa kwa uchaguzi mdogo.
Hata hivyo siku ya kukanushwa kwa kauli za Chama Cha Mapinduzi Diwani EZIRONI MWAKALOBO alisema kuwa uamuzi wa kujizulu umetokana na mvutano uliopo ndani ya Chama Chake.
WANAFUNZI WASHINDWA KUENDELEA NA MASOMO WILAYANI CHUNYA
Wanafunzi 400 waliotarajiwa kujiunga na shule mbalimbali za sekondari wilaya ya Chunya mkoani Mbeya mwaka huu wameshindwa kuendelea na masomo kutokana na sababu zisizojulikana.
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo MAURCE SAPANJO amesema wanafunzi hao licha ya kufaulu kwa viwango vizuri hawakuweza kuendelea na masomo na kwamba wazazi wa watoto wameshindwa kutoa ushirikiano kwa Serikali ili kufanikisha kuwarejesha wanafunzi hao masomoni.
Amesema uchunguzi uliofanywa na halmashauri hiyo umebaini kuwa watoto wengi wameshindwa kuendelea na masomo kwa sababu ya kukimbilia kwenye shughuli za madini.
Katika taarifa ya mkoa wa Mbeya iliyosomwa kwa Waziri mkuu MIZENGO PINDWA mwaka 2008 alipofanya ziara mkoani hapa ilidai kuwa wanafunzi 703 walikatiza masomo kwa sababu ya utoro na mimba.
TCRA YATOA MISAADA YENYE THAMANI YA MIL 2.5 WILAYANI CHUNYA.
Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA) Imetoa msaada wenye thamani ya Shilingi milioni kumi na mbili na nusu kwa ajili ya kununua computer, printer na photocopy katika shule za msingi na sekondari wilayani chunya.
Naibu mkurugenzi wa TCRA bwana VICTOR NKYA amesema misaada hiyo imetolewa ili iwawezesha wanafunzi na waalimu wa shule hizo kuendana na sayansi na teknolojia.
Wakati huohuo ameitaka Serikali kuongeza nguvu katika usambazaji wa vifaa vya teknolojia mshuleni ili kuwawezesha waalimu kuendana TEHAMA.
Shule zilizopata misaada hiyo ni Chunya kati, Chokaa, Mapogoro na Makongorosi ambapo kila shule imepata Computer moja na Printer moja.
MAUAJI YA KIMYA MKOANI MBEYA NI KAMA WIMBO WA TAIFA.
MBAGALE NDUNGA mwenye umri wa miaka 73 mkazi wa Chemchem Uyole ameuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni na watu wasiofahamika kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mchawi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ADVOCATE NYOMBI amesema marehemu alikuwa akituhumiwa kuhusika na matukio ya Uchawi ukiwemo wizi wa mazao shambani kwa njia za kishirikina.
Amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa Mbeya na upelelezi wa kuwabaini wahusika wa mauaji hayo unaendelea.
Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Mbeya mjini JOHN MWAMBIGIJA amesema pamoja na jitihada za uongozi wa chama chake kushinikiza kukanusha barua ya kujihuzulu wadhifa wake bado EZIRONI MWAKALOBO ameendelea na msimamo wake wa kung’atuka madarakani.
Aidha MWAMBIGIJA amesema mpango wa CHADEMA hivi sasa ni kujipanga katika kuhakikisha wanachukua tena kiti cha Udiwani kata hiyo mara baada ya kutangazwa kwa uchaguzi mdogo.
Hata hivyo siku ya kukanushwa kwa kauli za Chama Cha Mapinduzi Diwani EZIRONI MWAKALOBO alisema kuwa uamuzi wa kujizulu umetokana na mvutano uliopo ndani ya Chama Chake.
WANAFUNZI WASHINDWA KUENDELEA NA MASOMO WILAYANI CHUNYA
Wanafunzi 400 waliotarajiwa kujiunga na shule mbalimbali za sekondari wilaya ya Chunya mkoani Mbeya mwaka huu wameshindwa kuendelea na masomo kutokana na sababu zisizojulikana.
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo MAURCE SAPANJO amesema wanafunzi hao licha ya kufaulu kwa viwango vizuri hawakuweza kuendelea na masomo na kwamba wazazi wa watoto wameshindwa kutoa ushirikiano kwa Serikali ili kufanikisha kuwarejesha wanafunzi hao masomoni.
Amesema uchunguzi uliofanywa na halmashauri hiyo umebaini kuwa watoto wengi wameshindwa kuendelea na masomo kwa sababu ya kukimbilia kwenye shughuli za madini.
Katika taarifa ya mkoa wa Mbeya iliyosomwa kwa Waziri mkuu MIZENGO PINDWA mwaka 2008 alipofanya ziara mkoani hapa ilidai kuwa wanafunzi 703 walikatiza masomo kwa sababu ya utoro na mimba.
TCRA YATOA MISAADA YENYE THAMANI YA MIL 2.5 WILAYANI CHUNYA.
Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA) Imetoa msaada wenye thamani ya Shilingi milioni kumi na mbili na nusu kwa ajili ya kununua computer, printer na photocopy katika shule za msingi na sekondari wilayani chunya.
Naibu mkurugenzi wa TCRA bwana VICTOR NKYA amesema misaada hiyo imetolewa ili iwawezesha wanafunzi na waalimu wa shule hizo kuendana na sayansi na teknolojia.
Wakati huohuo ameitaka Serikali kuongeza nguvu katika usambazaji wa vifaa vya teknolojia mshuleni ili kuwawezesha waalimu kuendana TEHAMA.
Shule zilizopata misaada hiyo ni Chunya kati, Chokaa, Mapogoro na Makongorosi ambapo kila shule imepata Computer moja na Printer moja.
MAUAJI YA KIMYA MKOANI MBEYA NI KAMA WIMBO WA TAIFA.
MBAGALE NDUNGA mwenye umri wa miaka 73 mkazi wa Chemchem Uyole ameuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni na watu wasiofahamika kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mchawi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ADVOCATE NYOMBI amesema marehemu alikuwa akituhumiwa kuhusika na matukio ya Uchawi ukiwemo wizi wa mazao shambani kwa njia za kishirikina.
Amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa Mbeya na upelelezi wa kuwabaini wahusika wa mauaji hayo unaendelea.
Zimewekwa na UKURASA MPYA HUU http://ukurasampyahuu.blogspot.com/
Thursday, July 21, 2011
VIONGOZI WA NCHI MBILI WAKISHUHUDIA MAWAZIRI WAO WAKIBADILISHANA MIKATABA
Mawaziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na Tanzania Bernard Membe na Bi. Maite Nkoana Mashabane wakibalishana mikataba ya kuanzishwa kwa Tume ya Ushirikiano (Bi-National Commission) kati ya nchi hizo mbili muda mfupi baada ya kusaini katika ikulu ya Afrika ya Kusini jijini Pretoria jana huku marais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete na Jackob Zuma wakishuhudia.
RAIS KIKWETE ZIARANI AFRICA YA KUSINI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na jeshi la Ulinzi la Afrika ya Kusini wakati wa mwanzo wa Ziara yake Rasmi ya kitaifa nchini Afrika ya Kusini hivi karibuni.
NCHI WANACHAMA WA UMOJA WA MATAIFA WAPINGA BARAZA KUU LA USALAMA
NCHI WANACHAMA WA UMOJA WA MATAIFA WAPINGA BARAZA KUU LA USALAMA KUPEWA DHAMANA YA KURATIBU NA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI (1)
Wakati tishio la mabadiliko ya tabia nchi likiwa Dhahiri kwa hatima ya mataifa mbalimbali yakiwamo yale ambayo ni visiwa. Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wamepinga kwa mara nyingine, juhudi za Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa za kushinikiza kupewa dhamana ya kuratibu athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Kwa siku nzima ya jumanne, Baraza hilo ambalo liko chini ya Uraisi wa Ujerumani kwa mwezi huu wa Saba, lilikuwa na mjadala wa wazi kuhusu Udumishaji wa amani na usalama wa kimataifa; madhara ya mabadiliko ya tabia nchi.
Lengo la majadiliano hayo pamoja na mambo mengine,yalikuwa ni kwa Baraza hilo kushinikiza liwe na uwezo wa kuratibu na kushughulikia uwezekano wa ukosefu wa amani na usalama utakaosababishwa na madhara ya yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi.
Karibu kila Balozi anayeiwakilisha nchi yake katika UM ,wakiwamo baadhi ambao nchi zao ni wajumbe wa kudumu wa Baraza la Usalama maarufu kama P5, waliochangia majadialiano hayo, walisema ingawa wana kubali ukweli kwamba madhara ya mabadiliko ya tabia nchi, yanatishia usalama na amani ya jumuia ya kimataifa, bado Baraza hilo haliwezi kuwa na dhamana ya kulijadili , kulitolea maamuzi au maelekezo suala hilo.
Baadhi ya hoja zilizotolewa na wazungumzaji hao ni kwamba, ikiwa Baraza Kuu la Usalama litapewa dhamana hiyo. Siyo tu kwamba ,halina wataalam katika eneo hilo, lakini litakuwa linaingilia majukumu, dhamana na wajibu wa vyombo vingine vya UM ambavyo hasa ndivyo vilivyokasimiwa kulishughulikia tatizo hilo. Na kusisitiza kuwa viachwe vyombo hivyo vifanye kazi yake
Majadiliano hayo yalifunguliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, ambaye pamoja na kuwasilisha taarifa yake kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, lakini pia alisema, athari za mabadiliko hayo zipo wazi kabisa na wala hazina mjadala.
Hata hivyo akasema, yeye anadhani kutokana na tishio la kiusalama, na ustawi wa maendeleo na uhai wa mataifa mbalimbali na watu wake. Baraza Kuu la Usalama, linapashwa pia kupewa dhamana ya kuratibu athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Akichangia majadiliano hayo, mwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika UM, Balozi Ombeni Sefue, alisema , Serikali ya Tanzania inatambua kwamba kuna kipengele cha usalama katika mabadiliko ya tabia nchi, kipengele ambacho pia kiko karibu katika kila jambo katika dunia hii.
“ Hata hivyo hatujayaleta hayo mengine kujadiliwa katika Baraza Kuu la Usalama la UM kama tunavyotaka kufanya kwa hili. Ujumbe wangu unaamini kwamba, mabadiliko ya tabia nchi yanashughulikiwa kwa ukamilifu na vyombo vya msingi vya UM. Vyombo ambayo vimepewa dhamana ya kushughulikia suala la Maendeleo Endelevu ” akasema Balozi Sefue.
Na kuongeza. “Mwaka 2007 tulikuwa na majadiliano kama haya, na maoni ya wajumbe wengi waliochangia majadiliano yale yalikuwa, Baraza la Usalama lijiepushe kuingilia dhamana za taasisi nyingine za UM kama vile Mfumo wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi (UNFCCC ) na Baraza la Uchumi na Mandeleo ya Jamii ( ECOSOC).
Aidha Balozi Sefue amasema, Tanzania kama ilivyo kwa mataifa mengine inatambua ukubwa wa athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa visiwa vilivyoko katika bahari ya Pasifiki.
Lakini akasema , tishio la kutoweka kwa nchi hizo, tishio ambalo pia linaweza kuzalisha wakimbizi ,haliko kwa visiwa hivyo tu. Bali ni tishio hata kwa Tanzania n ambayo nayo ina visiwa ambavyo vimo hatarini kutoweka.
Kwa hiyo akasema , ndiyo maana Tanzania imekuwa ikisisitiza na kusimamia kwamba majadiliano kuhusu tatizo la mabadiliko ya tabia nchi na athari zake lijadiliwe zaidi katika ngazi ya kimataifa kupitia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ili kupata ufumbuzi wa kudumu.
Akasisitiza kuwa, kwa kutenga tatizo la mabadiliko ya tabia nchi na kuliingiza katika Baraza Kuu la Usalama, kunaweza kufifisha jitihada zote ambazo zimekwisha kufanyika na hivyo kutokamilisha majadiliano yanayo simamiwa na UNFCCC.
Halikadhalika , mwakilishi huyo wa Tanzania amerejea wito uliotolewa na wajumbe wengine wa kutaka nchi maskini kama Tanzania na zile ambazo zimo katika hatari kubwa ya kutoweka, na zile ambazo zimeonyesha nia thabiti ya kudhibiti hewa ukaa na uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti ya ziada. Zisaidiwe kwa hali na mali na mataifa yaliyoendelea ambayo hasa ndiyo chanzo kikubwa cha mabadiliko ya tabia nchi.
Subscribe to:
Posts (Atom)


